Last updated: February 8, 2010 :

TANZANIA, NCHI YETU

 

 

 

KAMA NINGEKUWA RAIS WA TANZANIA...

Ningehakikisha kuwa barabara ya Dar-Mwanza imejengwa kwa lami kurahisisha usafiri na kuunganisha zaidi ya raia millioni kumi wa nchi yangu kabla sijatumia mabilioni ya pesa kununua mashangingi kwa ajili ya wabunge na viongozi wa serikali. Ningehakikisha kuwa miundombinu ya kisiwa cha Pemba ni ya kiwango cha kuridhisha kabla sijatumia mabilioni kujenga majengo mawili mapya ya bunge. Ningehakikisha kuwa bandari tatu kubwa za Tanzania za; Unguja, Tanga, na Dar es salaam zimejengwa kwa kiwango cha kuridhisha kabla sijatumia mabilioni kununua ndege mbili za Raisi na rada mbovu. Kabla sijawaambia watanzania wenzangu kufunga mikanda kubana matumizi, ningepunguza mishahara ya wabunge kwa ku-veto miswada yao ya kujiongezea malipo kila mwaka. Kabla sija-sign bajeti ya serikali kuwa sheria, ningehakikisha kuwa mawaziri wanatoa maelezo ya uhakika kuhusu matumizi ya mabilioni ya fedha walizopewa kwa kipindi kinachoisha....[Habari Kamili >>]

_______________________________________________

MWALIMU'S ADVCE TO KIKWETE

And concerning mining policies: I'm sorry Jakaya, but I think you and your dumb MPs have no clue of what you are doing. You don't seem to have a clear goals here (at least not yet). I mean, Russia has tried and succeeded to assert more control over its oil and gas resources. Venezuela and Bolivia have moved to curtail oil companies; but in Tanzania, companies which mine gold, diamonds and other germs pay no corporate taxes, they only pay small sum of royalties and low wages to their workers. That makes no sense to me! Three decades ago, Batswanans were suffering exactly the same kind of probem Tanzanians are suffering now—exploitation from Western investors. But when Botswana government saw its reserves dwindling, it knew it had to do something. It tightened its belt, pulled together, renegotiated the mining contracts—and got through the crisis. I suggest you do the same. Send your economic advisers to Botswana so they can learn more on this matter because the current state of mining industry in Tanzania is too exploitive to be allowed to go on....[Full Story >>]

_______________________________________________

MMEA WA KIJANI NA MKANGANYO WA KISIASA

Tofauti na jirani zake (Kenya na Uganda), Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani zilizopiga marufuku utafunaji ama uraji wa miraa (Gomba,mirungi au Ghati kama ijulikanavyo) hadharani. Utakuwa umefanya kosa sawa tu na aliyekutwa akitumia madawa mengine ya kulevya kama vile coccaine na heroine endapo kama utakaidi sheria iliyopo na kuamua kufanya hivyo. Swali linabaki wazi: je, inawezekanaje nchi kama Tanzania yenye mtazamo tofauti kabisa na jirani zake wa Uganda na Kenya kuunda shirikisho na mataifa ya Afrika Mashariki wakati nchi hizo kama wadau halisi wa ushirikiano huo wananchi wake wanakula au kutafuna mirungi hadharani? Ni swali gumu linalohitaji majibu ya msingi. Na si majibu ya msingi tu, bali ufafanuzi yakinifu kuhusu kama Tanzania itaendelea na itikadi za kupinga utafunaji wa mirungi hadharani ama italegeza kamba na kuamua kuruhusu utafunaji wa mmea huo ya kijani hadharani....[Habari Kamili >>]

Linux web hosting - Get rock solid web hosting at Webquarry!

www.bongotz.com ©Copyright:BongoTz.Com -MMV. All Rights Reserved.